Queen Darleen Akanusha Tetesi za Kutoka Kimapenzi na Mbosso

Queen Darleen Apangua Tetesi za Kutoka Kimapenzi na Mbosso
Msanii  Queen Darleen ameeleza ni kwanini watu wamekuwa wakihisi ana mahusiano na Mbosso.

Muimbaji huyo pekee wa kike kutokea WCB amesema ni kwa sababu hajaweka wazi yupo kwenye mahusiano na nani.

"Kwa sababu hawamjui bwana wangu ndio sababu wanaongea lakini wangekuwa wanamjua wasingeongea na hawatamjua hadi niolewe," Darleen ameiambia SnS Tanzania (Simulizi na Sauti).

Kwa upande wake Mbosso alipoulizwa na waandishi kwenye red carpet ya Biko Jibebe Challenge alisema hakuna kitu kama hicho na kuulizwa swali kama hilo ni kuvunjiwa heshima.

0 comments:

Banner1

Banner1