Mwanamme ata kuchukia sana ukimfanyia mambo haya kitandani jifunze………???
– Wanaume wamejaa majisifu, hata awe anaumia kiasi gani atakaa
ngumu eti kwa sababu “mwanamume ni kuvumilia”. Kumbe mle ndani anakatika
maini Mwanamume atakuchukia sana ukimfanyia mambo haya kitandani
Wanaume wanahofia sana kuonekana bwege chumbani. Wanasayansi wamefanya
tafiti kadha na kuhitimisha kuwa wanaume wanaogopa sana kuachwa na
mchumba na pia kudhalilishwa.
Eneo moja ambalo wanaume wanahofia zaidi
ni kuonekana duni kitandani. Wanatatizika kila wanapofikiria kuwa ustadi
wao uwanjani ni wa ligi ya chini; kwamba hawawezi kukufikisha kileleni
ilhali unawapa mahaba ya kutosha. Itakuwa vyema kwako mwanadada
kuhakikisha kuwa unamuondolea mpenzi wako mawazo haya ya kumfedhehesha.
Chukua hatua zifuatazo:
1. Usimlinganishe na wengine.
Yawezekana umekuwa na mchumba mmoja tu, ama yeye ni wa mia moja!
Kwanza, usithubutu kumtajia idadi hiyo. Pili, usimlinganishe hata chembe
na hao wengine wa zamani isipokuwa tu kama yeye ndiye ameibuka bora
kuliko wote!
2. Usimkashifu
Hakuna aliye kamili;mpenzi wako atashindwa na mechi nyakati
zingine. Usimuonyeshe kadi nyekundu, subiri mechi iishe ama aondoke kwa
utaratibu. Siku ambazo itakubidi ujifanye umefika kileleni, acha iwe ni
siri yako mwenyewe; kama wasemavyo, hakuna siri ya wawili! Utamfaa zaidi
wakati wa mechi ukimuelekeza kwa upole, hatimaye atatinga bao!
Mwanamume atakuchukia sana ukimfanyia mambo haya kitandani Utamu wa
mapenzi ni kubadilisha mitindo na usukani
3. Usiwe wa kupewa tu
Mazoea hayana raha hususan iwapo mwanamume wako anachemsha kila
mnaporejelea mtindo ule ule. Utamu wa mapenzi ni kubadilisha mitindo
mara kwa mara, kubuni njia zenu za kipekee kulishana mahaba. Kumbuka
kuwa hakuna bingwa kitandani, mara kwa mara chukua usukani umuonyeshe
mambo mapya!
4. Usilete vita chumbani
Chumbani ni pahali pa kujituliza, kufungua roho yako na kujumuika
pamoja na mpenzi wako kuleta raha. Vita nje na uweke kando mabishano
yoyote; vile vile, majadiliano yasiyohusu shughuli mnayotekeleza, kama
kupanda kwa gharama ya maisha. Mpe mapenzi atosheke na hakika ataondoa
hofu zake.
0 comments: